Friday 8 August 2008

WENGER AFURAHIA RONALDO KUBAKI MAN U!
REAL WASHUSHUKA, WAFUNGA MIDOMO!
Arsene Wenger amesema amefurahishwa na habari kwamba Cristiano Ronaldo atabaki Manchester United.
Amesema: ‘Nimefurahi kwa sababu anatuletea vitu spesho kwenye LIGI KUU. Tunataka iwe ligi bora duniani hivyo ni muhimu wachezaji bora wacheze hapa. Nimefurahi sakata hili limeisha kwa busara na watu wameheshimu mikataba. Ingesikitisha sana kumuona mmoja wa wachezaji bora duniani akidharau mkataba na kuondoka tu!’
Wakati huohuo, Rais wa Real Madrid, Ramon Calderon, amedai hajui kama Ronaldo amewashushua na akaongeza hataki kuongea lolote kuhusu mchezaji huyo!

Nae Meneja wa Real Bernd Schuster amesema: ’Inasikitisha kwani ni mchezaji ambae angetuinua sana! Lakini hatujali! Tuna kundi la wachezaji wazuri hapa.’

No comments:

Powered By Blogger