Thursday 7 August 2008

Refa wa LIGI KUU UINGEREZA Mark Clattenburg asimamishwa!!
-ALIKUWA ACHEZESHE MECHI YA NGAO YA HISANI YA MAN U vs PORTSMOUH JUMAPILI!!!!
Chama cha Soka Uingereza [FA] na Bodi ya Marefa wa Kulipwa [PGMO] vimetangaza kumsimamisha Refa anaechezesha LIGI KUU UINGEREZA Mark Clattenburg kutokana na Kampuni zinazohusiana na yeye kupigwa mufilisi kisheria.


FA na PGMO vimesema imekuwa ni busara Refa huyo asimamishwe ili uchunguzi wa kina ufanyike kuhusu madeni na kufilisika kwa kampuni zake ili hadhi ya Soka Uingereza isitiwe dosari.
Mark Clattenburg alipangwa kuchezesha mechi ya Jumapili tarehe 10 Agosti 2008 ya ufunguzi rasmi wa msimu wa 2008/9 wa Soka Uingereza kugombea NGAO YA HISANI kati ya Mabingwa wa LIGI KUU MAN U na Mabingwa wa Kombe la FA PORTSMOUTH itakayochezwa Uwanja wa Wembley.

Nafasi ya Refa huyu kuchezesha mechi hiyo itachukuliwa na Peter Walton.

No comments:

Powered By Blogger