Friday 8 August 2008

CHELSEA WATOA KITITA KUMNUNUA ROBINHO!!!
Chelsea wametangaza wametoa ofa ya Pauni milioni 19 kwa Real Madrid ili kumnunua Winga wa Brazil Robinho.

Inasemekana Robinho hana furaha Real na ukweli ni kwamba tangu ahamie hapo hana namba ya kudumu.
Endapo Chelsea watafanikiwa kumchukua Robinho basi huyu atakuwa Mbrazil wa pili kutua hapo tangu Meneja Mbrazil Scolari aanze kazi Chelsea.

Wa kwanza ni Mchezaji wa Ureno aliezaliwa Brazil Deco aliesainiwa kwa dau la Pauni milioni 8 kutoka Barcelona.

No comments:

Powered By Blogger