Tuesday 5 August 2008

Blackburn wamchukua kinda wa Man Utd Simpson
Beki chipukizi wa Man U Danny Simpson ameenda Blackburn Rovers kwa mkopo.
Simpson [21] alicheza Man U mechi 8 msimu uliopita na ameshawahi kuchezea kwa mkopo timu za Sunderland, Ipswich na klabu ya Ubelgiji Royal Antwerp.
Mpaka sasa, Blackburn ishawasaini wachezaji watatu kwa msimu ujao na wengine ni aliekuwa Kipa wa Uingereza Paul Robinson na Carlos Villanueva.
Drogba ATAKOSA MWANZO WA LIGI
Didier Drogba[30] atakosa kucheza mwanzo wa msimu kutokana na kuuguza goti alilofanyiwa operesheni. Taarifa hii imethibitishwa na Meneja wa Chelsea Scolari ambae amesema hatochezi mechi ya kwanza ya msimu dhidi ya Wigan tarehe 16 Agosti 2008 lakini inawezakana akacheza mechi ya pili na Tottenham tarehe 31 Agosti 2008.
Scolari ametamka Niicolas Anelka atacheza nafasi ya Drogba.

No comments:

Powered By Blogger