Tuesday 5 August 2008

Van Nistelrooy astaafu kuchezea UHOLANZI!!!
Mshambuliaji mahiri Mholanzi anaechezea Real Madrid, Ruud van Nistelrooy [32], ametangaza kustaafu kuichezea Timu ya Taifa ya Uholanzi aliyoanza kuichezea mwaka 1998 na kuifungia magoli 33 na kumfanya kuwa Mfungaji Bora wa 3 katika historia ya timu hiyo.
Hakucheza EURO 2000 kutokana na kuwa majeruhi lakini alicheza na kufunga kwenye EURO 2004, EURO 2008 na Kombe la Dunia mwaka 2006.
Ruud van Nistelrooy alijijengea jina alipokuwa Klabu ya PSV Eindhoven ingawa aliumia vibaya goti lakini hilo halikumzuia Sir Alex Ferguson kumchukua kwenda MAN U mwaka 2001 kwa Pauni milioni 19 na kuweka rekodi ya Uingereza ya kununua mchezaji kwa bei ghali kwa wakati huo.
Alikaa MAN U kwa miaka mitano iliyojaa mafanikio makubwa na mwaka 2006 akahamia Real Madrid kwa dau la Pauni milioni 10.

No comments:

Powered By Blogger