Friday 8 August 2008



FERGUSON: NI VIGUMU RONALDO KUHAMA

Baada ya kuhakikisha Cristiano Ronaldo anabakia kuwa mchezaji wa Man U, Sir Alex Ferguson anahisi Winga huyo wa Ureno ataona shida sana kuihama klabu hiyo kadri anavyozidi kukaa.
‘Tuna furaha.’ Bosi huyo alitamka leo. ‘Kama nilivyosema ishu hii imekufa. Yeye ni mchezaji wa Manchester na ana furaha kuwa hapa. Ni basi tu hawa Real walijaribu kumrubuni na kufanya maisha yake kuwa magumu.’
Ferguson aliongeza: ‘Kitu muhimu tumemaliza huu upuuzi wa Real. Kadri anavyokua ndio ataridhika kuwa hapa. Hii siku zote imetokea kwa wachezaji wanaokuwa hapa muda mrefu. Hawataki kuondoka!’
‘Mtizame Rio Ferdinand aliejiunga nasi akiwa mdogo tu kutoka Leeds United! Leo ni mchezaji wa kweli kweli wa Manchester United! Anaipenda klabu kwa moyo wote! Na Rio anatoka nchi nyingine…….anatoka London! Ni dunia nyingine kule! Hamna tofauti kati ya mtu anaehama London au Ureno na kuja Manchester. Unakuja hapa ni baridi sana, mvua nyingi! Lakini unakuja kwenye mji wa soka na miji mingi si hivi!’
Ferguson akamalizia: ‘Sasa Real wanatambua wanapambana na mnyama mwingine kabisaa!’

RONALDO: FERGUSON NI KAMA BABA YANGU WA PILI!
Nae Ronaldo alipohojiwa anahisi nini kuhusu imani ya Sir Alex Ferguson kuwa hahami Man U, alijibu: ‘Niamini kabisa, najisikia mwenye majivuno sana kujua Sir Alex ananithamini sana. Na yeye anajua namthamini sana. Yeye ni mtu muhimu sana katika maisha yangu. Si kwa sababu ya niliyojifunza kwake na ambayo ntaendelea kujifunza lakini vilevile ni kwa utu na ubinadamu wake. Ana hisia kubwa katika soka. Kama inawezekana basi maisha yote ningependa abaki na mimi na awe karibu yangu. Najua haiwezekani lakini yeye siku zote amekuwa kama baba yangu wa pili. Sitosahau aliponikabidhi jezi ya MAN U yenye namba 7 na kuniambia maana yake [Namba 7 Man U ilivaliwa na nyota George Best na Bryan Robson]. Daima itakuwa namba yangu. Sir Alex Ferguson amekuwa mtu muhimu katika maisha yangu ya soka. Kwa sababu hiyo, na kwa sababu tuna uhusiano wa karibu sana, najua anafahamu vizuri sana wakati gani awe na wasiwasi na nini kilicho bora kwa mwanawe.’

No comments:

Powered By Blogger