Friday 8 August 2008

FERGUSON APINGA VIKWAZO KWA WACHEZAJI WASIO RAIA WA UINGEREZA LIGI KUU
Sir Alex Ferguson amewasihi viongozi wa Soka wa Uingereza wasiburuzwe katika kuweka vikwazo kwa wachezaji kutoka nje ya Uingereza kuchezea LIGI KUU UINGEREZA.
Meneja huyu wa Manchester United akiandika utangulizi wa gazeti rasmi la ufunguzi wa msimu wa 2008/9 wa LIGI KUU UINGEREZA alihoji: ‘Kwa nini uhangaike kutengeneza kitu wakati hakijaharibika?’
"Kumekuwa na lawama kwenye vyombo vya habari na wito wa kuweka idadi maalum ya Wachezaji wasio Waingereza kucheza mechi ili kuhakikisha Waingereza wanapata namba.’ Aliandika Ferguson. ‘Mimi sikuchezesha Wachezaji 6 Waingereza kwenye Fainali ya LIGI YA KLABU BINGWA ULAYA kwa sababu tu za kisiasa mie niliwachagua wale kwa sababu tu walikuwa na uwezo wa kunyakua Kombe hilo.’
Alikuwa akimaanisha Wachezaji Waingereza 6 wa MAN U walioanza Fainali ya LIGI YA KLABU BINGWA ULAYA walipowafunga Chelsea. Wachezaji hao ni Wes Brown, Rio Ferdinand, Owen Hargreaves, Michael Carrick, Paul Scholes na Wayne Rooney.
FIFA imeshika bango ikitaka Wachezaji wasio raia wawekewe vikwazo kwenye LIGI KUU UINGEREZA hali ambayo inaelekea kuungwa mkono na UEFA na FA, Chama Soka Uingereza.
Lakini Ferguson anapinga hilo na kudai wageni hawazuii Waingereza kujitokeza na kuonyesha umahiri wao na anaonya hatua hiyo ya FIFA, UEFA na FA huenda ikaibomoa LIGI KUU UINGEREZA kutoka ligi bora, ngumu na yenye sifa duniani kitu kilichodhirishwa na kuwa na Timu 4 kwenye Nusu Fainali ya LIGI YA KLABU BINGWA ULAYA msimu uliopita na hatimaye Kombe kuchukuliwa na Timu ya Uingereza-Manchester United.
......................KUHUSU RONALDO FERGUSON ASEMA:
'Kadri anavyokua ndio atajua na kukubali na kuridhika kwamba Man U ndio klabu anayostahili kuwepo. Mtizame Rio Ferdinand. Sasa humbandui hapa. Lakini nimefurahi sana upumbavu huu wa Real Madrid umekwisha. Sasa wanajua vizuri wanapambana na watu gani!'

No comments:

Powered By Blogger