Thursday 7 August 2008

UHAMISHO LIGI KUU UINGEREZA
Fulham wamemchukua Mshambuliaji Andy Johnson kutoka Everton kwa dau la Pauni milioni 10 na nusu.
Andy Jonhson ilikuwa asaini mkataba tangu mwezi uliokwisha lakini kukawa na mzozo baada ya matokeo ya kupimwa afya kuonyesha goti lake sio timamu na kuwatia kiwewe Fulham na ikabidi wawalazimishe Everton wapunguze ada waliyoitaka ya Pauni milioni 12.
Jonhson sasa amesaini mkataba wa miaka minne.
=============================================
Aston Villa wamekubaliana na Middlesbrough ili wamnunue Mlinzi Luke Young ambae msimu uliopita alinunuliwa na Middlesbrough kutoka Charlton kwa ada ya Pauni milioni 2 na nusu.
Aston Villa watalipa Pauni milioni 5 kumchukua mchezaji huyo.
=============================================
Klabu Klabu ya Deportivo La Coruna ya Spain imetangaza mchezaji wake Fabricio Coloccini anahamia Newcastle.
Coloccini [26] ni Mlinzi kutoka Argentina na alitishia kuishitaki Deportivo La Coruna kama klabu hiyo haimruhusu kuhama.
=============================================
West Ham imemwachia huru Kiungo Freddie Ljungberg [31] baada ya makubaliano kufikiwa kukatisha mkataba wake.
Mchezaji huyu wa zamani wa Kimataifa wa Sweden na Arsenal huenda akastaafu soka kwa sababu ya kuumia.
Alijiunga na West Ham kutoka Arsenal Julai 2007 kwa ada ya Pauni milioni 3 na kwa mkataba wa miaka minne.
Msimu aliopita alicheza mechi 22 kati ya mechi 38 za LIGI KUU kwani aliandamwa na kuumia mara kwa mara. Mara ya mwisho alivunjika mbavu.
Alicheza EURO 2008 akiwa Nahodha wa Sweden na alitangaza kujiuzulu kucheza mechi za Kimataifa mara tu baada ya Sweden kutolewa mashindano hayo.
=============================================
Bolton wamesaini mkataba wa kumnunua Mnigeria mlinzi Danny Shittu [27] kutoka Klabu ya daraja la chini Watford kwa dau ambalo halikutangazwa.
Mnigeria huyu amechezea Timu ya Taifa ya Nigeria mechi moja na awali alishachezea klabu za QPR na Charlton zote za Uingereza.
=============================================
Blackburn imemsaini mdogo wake Mshambuliaji wao hatari kutoka Paraguay Roque Santa Cruz.
Julio Santa Cruz [18] ametoka Klabu ya Paraguay iitwayo Cerro Porteno na atajiunga na Blackburn Rovers mara tu baada ya kupata kibali cha uhamisho cha kimataifa.

No comments:

Powered By Blogger