Wednesday 6 August 2008

SAKATA LA RONALDO LAISHA!!!!!
Bosi wa Manchester United Sir Alex Ferguson ametamka jana kuwa sakata la Cristiano Ronaldo kuhama sasa limekwisha na winga huyo atabaki OLD TRAFFORD.
Tangu kuisha Fainali ya LIGI ya KLABU BINGWA ULAYA mwezi Mei ambayo Man U walitawazwa kuwa Mabingwa wa Ulaya, uvumi ambao hasa ulichochewa na Real Madrid ulizagaa kwamba Ronaldo atanunuliwa na klabu hiyo ya Spain.
Ronaldo jana alirudi Manchester baada ya mapumziko na vilevile kujiuguza baada ya operesheni ya enka aliyofanyiwa Amsterdam, Uholanzi mwezi uliopita.
Habari hizi za Ronaldo kubaki Man U zinathibitika kwa kauli ya Rais wa Real Madrid Ramon Calderon aliyoitoa jana hiyo aliposema: ‘Rafael van der Vaart ni mchezaji pekee tutakae msaini msimu huu’.
Jana hiyohiyo Real ilimtambulisha rasmi mchezaji huyo wa Kiholanzi Rafael van der Vaart iliemnunua kutoka Hamburg ya Ujerumani.
Sir Alex Ferguson alimaliza sakata hili lililodumu tangu Mei kwa msisitizo: ‘Jambo hili limekwisha. Yeye ni mchezaji wa Manchester United-mwisho! Atacheza hapa msimu ujao.’
Cristiano Ronaldo ana mkataba unaoisha mwaka 2012 na alisaini mkataba huu wa sasa mwaka jana tu.
.....NA ROONEY MGONJWA!!
Mshambuliaji Wayne Rooney huenda akaikosa mechi ya ufunguzi ya LIGI KUU UINGEREZA ya tarehe 17 Agosti wakati Man U itakapocheza na Newcastle kwa sababu ni mgonjwa.
Sir Alex Ferguson alisema jana: ’Sidhani kama Rooney atakuwa fiti. Aliugua tulipokuwa Nigeria na hajafanya mazoezi tangu wakati huo.’
Kuugua kwa Rooney ni tatizo kubwa kwa Man U kwani Ronaldo hatakuwepo uwanjani kwa takriban miezi miwili baada ya operesheni, Nani amefungiwa mechi mbili kwa kupewa kadi nyekundu msimu uliokwisha, Anderson yuko na Timu ya Brazil huko Beijing kwenye Olympic na Saha ni majeruhi.
Hivyo, Man U imebakiwa na fowadi mmoja tu- Carlos Tevez.
Inategemewa chipukizi Frazier Campbell [20] ataingizwa
kikosi cha kwanza kuleta sapoti.

No comments:

Powered By Blogger