Saturday 2 August 2008



Ole Gunnar Solskjaer aagwa OLD TRAFFORD!
MAN U 1 ESPANYOL 0
Akicheza dakika 25 za mwisho, leo Jumamosi, Agosti 2, 2008, Ole Gunnar Solskjaer aliagwa rasmi kuchezea MAN U katika mechi mahsusi iliyoandaliwa kwa ajili yake dhidi ya ESPANYOL ya Spain.
Katika mechi hii MAN U walipata bao lao la ushindi katika dakika ya 82 mfungaji akiwa chipukizi Frazier Campbell.
Ole Gunnar Solskjaer, umri miaka 35, alilazimika kustaafu soka Agosti 2007 baada ya kuumia goti.
Mechi ya kumuaga ilichezwa nyumbani kwa MAN U Uwanja wa OLD TRAFFORD na ilihudhuriwa na Watazamaji 68,868.
MAN U iliwakilishwa na wachezaji wafuatao [kwenye mabano ni wachezaji wa akiba walioingizwa pamoja na dakika waliyoingia]:
Van der Sar (Kuszczak 46); Simpson, Ferdinand (Brown 46), Vidic (Evans 62), Evra (Silvestre 46); Gibson (O’Shea 62), Fletcher, Scholes, Nani (Campbell 46); Giggs, Tevez (Solskjaer 68)

No comments:

Powered By Blogger