Thursday 31 July 2008



UHAMISHO LIGI KUU UINGEREZA: Tottenham wamnunua Bentley
Tottenham wamemsaini kiungo David Bentley kutoka Blackburn Rovers kwa thamani ya Pauni milioni 18.
Mwenyekiti wa Blackburn Rovers John Williams ametamka kuwa Bentley alipasi vipimo vya afya siku ya Jumatano na Klabu ya Tottenham leo itatoa tamko rasmi kuhusu uhamisho huu.
Bentley [23], ambae pia huchezea Timu ya Taifa ya Uingereza, aliingia Blackburn mwaka 2006 akitokea Arsenal na ameifungia Blackburn magoli 13 katika mechi 102 za LIGI KUU UINGEREZA. Pia ameshaichezea Timu ya Taifa ya Uingereza mara 6.
Tottenham mpaka sasa imeshawauza Paul Chimbonda, Teemu Tainio, Steed Malbranque [wote wamehamia Sunderland] na Kipa Paul Robinson alieenda Blackburn. Na mpaka sasa imewanunua mshambuliaji Giovani Dos Santos, kiungo Luca Modric na Heurelho Gomes.
.......................Na Newcastle wamchukua Bassong
Mlinzi wa Klabu ya Ufaransa Metz, Sebastien Bassong ambae pia ni mchezaji wa Timu ya Taifa ya Ufaransa ya Vijana chini ya miaka 21, amejiunga na Newcastle.
Bassong alikuwemo kwenye kikosi cha Newcastle kinachojitayarisha kwa msimu ujao ingawa alikuwa hajahama rasmi.
Sasa imethibitishwa Bassong ni mchezaji halali wa Newcastle.

No comments:

Powered By Blogger