Friday 1 August 2008

SOKA: OLYMPIC BEIJING 2008
Mashindano ya OLIMPIKI ambayo safari hii yanachezwa nchini China na yanajulikana kama OLYMPIC BEIJING 2008 yataanza wiki ijayo kwa michuano katika michezo ya kila aina.
Katika soka mechi zitaanza kuchezwa tarehe 7 Agosti 2008 na timu zilizofuzu kuingia OLYMPIC BEIJING 2008 ni:
-AFRICA: CAMEROON, NIGERIA, IVORY COAST
-ASIA: AUSTRALIA, JAPAN, CHINA, JAMHURI YA KOREA
-ULAYA: UBELGIJI, UHOLANZI, ITALIA, SERBIA
-MAREKANI KASKAZINI & KATI: HINDURAS, USA
-OCEANIA: NEW ZEALAND
-MAREKANI KUSINI: ARGENTINA, BRAZIL
Timu hizi zimegawanywa katika makundi manne ya timu 4 kila kundi na zitacheza kwa mtindo wa ligi na timu mbili za juu zitaingia raundi inayofuata.
Makundi ni:
KUNDI A: IVORY COAST, ARGENTINA, AUSTRALIA, SERBIA
KUNDI B: UHOLANZI, NIGERIA, JAPAN, USA
KUNDI C: CHINA, NEW ZEALAND, BRAZIL, UBELGIJI
KUNDI D: KOREA, CAMEROUN, HONDURAS, ITALY
Kufuatana na taratibu za FIFA, wachezaji wanaoruhusiwa kucheza michuano hii ni lazima wawe chini ya umri wa miaka 23 ingawa kila timu inaruhusiwa kuwa na wachezaji watatu wenye umri wa zaidi ya miaka 23.
Wachezaji nyota na maarufu ambao wataonekana uwanjani kwenye michuano hii ni pamoja na Ronaldinho, Anderson, Pato [wakiwakilisha Brazil], Riquelme, Lionel Messi, Macherano [Argentina], Ryan Babel [Uholanzi].

No comments:

Powered By Blogger