Monday 28 July 2008

BARTON AFUNGULIWA JELA!
Mchezaji kiungo wa Newcastle Joey Barton [pichani akitoka geti la jela leo asubuhi] ameachiwa kutoka jela baada ya kutumikia kifungo cha siku 74 katika adhabu yake ya kufungwa miezi 6 baada ya kupatikana na hatia ya kumpiga na kumjeruhi kijana mmoja nje ya hoteli mjini Liverpool Desemba 27 mwaka jana.
Barton alilakiwa nje ya geti la gereza na rafiki yake mmoja na alikataa kuongea na waandishi habari.
Jana Meneja wa Newcastle, Kevin Keagan, alitamka Joey Barton ataendelea kuichezea klabu hiyo ili kumpa nafasi kujirekebisha kinyume na fikra za wengi kuwa atafukuzwa klabuni.
Wakati akiwa kifungoni, Barton alipatikana na hatia katika kesi nyingine alipompiga na kumjeruhi mchezaji mwenzake wakati akiwa Manchester City.
Mfaransa Ousmane Dabo alipigwa na Barton kwenye mazoezi na kitendo hicho kilisababisha ahamishwe Manchester City na kwenda Newcastle.
Barton alikwepa jela kwenye kesi hii baada ya kuhukumiwa kifungo cha nje cha miezi minne.

No comments:

Powered By Blogger