Sunday 27 July 2008

Keegan ampa mchezaji mfungwa Barton nafasi kujirekebisha!!!!
Meneja wa Newcastle Kevin Keegan amesisitiza ni haki na ubinadamu kumpa Mchezaji wake alie jela nafasi ya kujirekebisha kwa kumruhusu kuendelea kuichezea Newcastle atakapofunguliwa.
Kiungo Joey Barton alihukumiwa kifungo cha miezi 6 jela baada ya kupatikana na hatia ya kushambulia na kumjeruhi kijana mmoja nje ya hoteli mjini Liverpool. Adhabu yake hiyo inaisha wiki ijayo na hatua ya Keegan kumsamehe imezima dhana na uvumi kuwa mchezaji huyo mwenye historia ya ukorofi atafukuzwa.
Wakati akitumikia kifungo hiki cha miezi 6 Barton alipatikana na hatia ya kumjeruhi mchezaji mwenzake kwenye kesi nyingine wakati alipokuwa Manchester City. Mfaransa Ousmane Dabo alipigwa na Barton kwenye mazoezi na kitendo hicho kilisababisha ahamishwe Manchester City na kwenda Newcastle. Barton alikwepa jela kwenye kesi hii baada ya kuhukumiwa kifungo cha nje cha miezi minne.

No comments:

Powered By Blogger