Wednesday 30 July 2008

SAHA KUHAMISHWA MAN UNITED?
Luis Saha ni mchezaji kipenzi wa mashabiki wengi wa Man U hasa kwa umahiri na ustadi wake wa kushambulia na kufunga magoli lakini wengi wanahuzunika sana kwa jinsi anavyoandamwa na maumivu ya mara kwa mara na kumfanya acheze kwa nadra sana.
Luis Saha alicheza mechi 24 tu msimu uliopita alioandamwa mfululizo na majeruhi hasa goti lililomsumbua muda mrefu sana.
Inasemekana Meneja wa Man U, Sir Alex Ferguson, ameshakata tamaa kuhusu Saha na yuko tayari kumuuza.
Tayari Klabu za Fulham, Bolton, Roma, Paris St Germain na Monaco zinapigana vikumbo kumnunua ingawa wengi wanaamini ataenda kwa Kepteni wa zamani wa Man U, Roy Keane, kwenye timu ya Sunderland.
Kuuzwa kwa Saha kunaonekana hakuepukiki hasa ikizingatiwa Man U inamuwania Dimitar Berbatov wa Tottenham ingawa vilevile inadaiwa washambuliaji wengine wanatajwa kuwemo kwenye listi ya wachezaji wanaowindwa na Man U.
Listi hiyo ina majina ya Roque Santa Cruz wa Blackburn Rovers, Klaas Jan Huntelaar wa Ajax na hata Thierry Henry yumo!!

No comments:

Powered By Blogger