Monday 28 July 2008


MAN U WASHINDA TENA AFRIKA!!!!!!!!!!!!!!!!

MAN U 2 PORTSMOUTH 1

Wakicheza mechi yao ya pili ndani ya siku mbili barani Afrika, MAN U leo wameifunga timu ya LIGI KUU UINGEREZA PORTSMOUTH mabao 2-1 katika UWANJA WA TAIFA mjini Abuja, Nigeria.

Jana, Man U walicheza Pretoria, Afrika Kusini na kuwafunga wenyeji wao Kaiser Chiefs 4-0 na kutwaa Kombe la VODACOM.

Katika mechi ya leo, mabao ya Man U yalifungwa na Chris Eagles na Carlos Tevez. Bao la Portsmouth lilifungwa na Jermaine Defoe.

Timu hizi zitakutana tena katika mechi ya kufungua pazia msimu mpya wa mwaka 2008/9 wa Uingereza kwa kushindania NGAO YA HISANI Uwanja wa Wembley, tarehe 10 Agosti 2008.

Timu hizi zinakutana kwa sababu Man U ni Bingwa wa LIGI KUU na Portsmouth ndie alieshinda Kombe la FA.

No comments:

Powered By Blogger