Friday 1 August 2008

ARSENAL KUIKWAA TIMU YA MENEJA WA ZAMANI UINGEREZA STEVE McCLAREN!!!!
UEFA wametangaza timu zitakazopambana kwenye Raundi ya Tatu ya Mtoano katika mashindano ya LIGI YA KLABU BINGWA ZA ULAYA baada ya kupigwa kura.
Katika raundi hii mechi zitachezwa tarehe 12 na 13 Agosti na marudiano ni tarehe 26 na 27 Agosti kwa mtindo wa nyumbani na ugenini.
Arsenal imepangwa kukutana na timu ya Uholanzi FC Twente inayoongozwa na aliekuwa Meneja wa Timu ya Taifa ya Uingereza Steve McClaren ambae alitimuliwa kazi hiyo Novemba 2007.
Liverpool itakutana na Standard Liege ya Ubelgiji.
Mechi zimepangwa kama ifuatavyo:
Anorthosis au Rapid Vienna v Olympiakos

Vitoria Guimaraes v IFK Gothenburg au BaselShakhtar

Donetsk v Domzale au Dinamo Zagreb

Schalke 04 v Atletico Madrid

Aalborg au Modrica v RANGERS au Kaunas

Barcelona v Beitar Jerusalem au Wisla Krakow

Levski Sofia v Anderlecht au BATE

Standard Liege v LIVERPOOL

Inter Baku au Partizan v Fenerbahce au MTK Budapest

FC Twente v ARSENAL

Spartak Moscow v Drogheda au Dinamo Kiev

Juventus v Tampere au Artmedia

SK Brann au Ventspils v Marseille

Fiorentina v Slavia Prague

Galatasaray v Steaua Bucharest

Panathinaikos au Dinamo Tbilisi v Sheriff Tiraspol au Sparta Pragu

Washindi 16 wa mechi hizi watajumuika na timu nyingine 16 ambazo ni Mabingwa wa Nchi na washindi wa pili wa ligi za nchi [Timu kutoka Uingereza ni Mabingwa Man U na washindi wa pili Chelsea] kufanya jumla ya timu 32 zitakazogawanywa makundi manane ya timu 4 kila moja zitakazocheza mtindo wa ligi.Mechi hizi za makundi zitaanza tarehe 16 Septemba na kumalizika Desemba 10.

No comments:

Powered By Blogger