Sunday 27 July 2008

MAN U WAUA BONDENI!
Man U jana walitwaa Kombe la Vodacom kwenye Uwanja wa Loftus huko Pretoria, Afrika Kusini walipowabamiza Kaiser Chiefs kwa mabao 4-0.
Wakichezesha timu yenye mchanganyiko wa chipukizi na mastaa wao wa kila siku, Man U walifunga mabao kupitia mkongwe Giggs, dakika ya 40, staa Rooney, dakika ya 57, machipukizi Cleverley, dakika ya 62 na Frazier Campbell, dakika ya 86.
Leo, Man U wako nchini Nigeria watakapokumbana na timu nyingine ya LIGI KUU UINGEREZA Portsmouth kwenye mechi ya kirafiki.

No comments:

Powered By Blogger