Wednesday 30 July 2008


ARSENAL WAMSAJILI BISCHOFF
Arsenal wamethibitisha kwamba wamemsaini Kiungo wa Klabu ya Ujerumani Werder Bremen Amaury Bischoff, mwenye miaka 21, ambae ingawa alizaliwa Ufaransa huichezea Timu ya Taifa ya Vijana wa chini ya miaka 21 ya Ureno.
Bischoff hakuwa akichezeshwa mara kwa mara alipokuwa Werder Bremen lakini Arsene Wenger anaamini ana kipaji kitakachoisaidia Arsenal hapo baadae.
Bischoff atavaa jezi namba 28 akiwa Arsenal na inasadikiwa ataziba mapengo yaliyoachwa na Viungo Mathieu Flamini, Gilberto na Alexander Hleb waliohama timu.

No comments:

Powered By Blogger