Wednesday 30 July 2008


KINDA WA MAN U AJIUNGA BURNLEY
Mchezaji chipukizi wa Man U, Chris Eagles, ambae aling’ara katika ziara ya Afrika ya Man U ya hivi juzi alipofunga magoli katika mechi dhidi ya Kaiser Chiefs huko Afrika Kusini na Portsmouth mjini Abuja, Nigeria, amehamia timu ya Burnley inayochezea kwenye LIGI YA COCA COLA ambayo ni ligi chini tu ya LIGI KUU UINGEREZA.
Chris Eagles, mwenye umri wa miaka 22, alieanza kuichezea Man U tangu akiwa na miaka 14 ameshindwa kupata namba ya kudumu kwenye kikosi cha kwanza cha Man U na muda mwingi aliishia kupelekwa kucheza kwa mkopo kwa timu nyingine.
Timu alizowahi kucheza kwa mkopo ni Watford, Sheffield Wednesday na Klabu ya Uholanzi ya NEC Nijmegen.

LEE CATTERMOLE AENDA WIGAN
Kiungo wa Middlesbrough, Lee Cattermole, miaka 20, anaechezea Timu ya Taifa ya Uingereza ya Vijana wa chini ya miaka 21, amesaini mkataba wa miaka mitatu kujiunga na Wigan kwa dau ambalo halikutangazwa.
Mpaka sasa Wigan imeshanunua wachezaji Olivier Kapo na Daniel de Ridder kutoka Birmingham City na imemchukua mchezaji wa Misri mshambuliaji Amr Zaki kutoka Klabu ya Zamalek kwa mkopo wa mwaka mmoja.

No comments:

Powered By Blogger