Monday 28 July 2008




UHAMISHO LIGI KUU UINGEREZA

Mshambuliaji wa Everton Andy Jonhson yuko njiani kuhama na inasemekana leo amepimwa afya yake kwenye Klabu nyingine ya LIGI KUU UINGEREZA Fulham.

Nae Robbie Keane wa Tottenham anaripotiwa kuwa atachukuliwa na Liverpool kwa dau la Pauni milioni 20. Mazungumzo ya uhamisho huu yanadaiwa yako hatua za mwisho.
Inasemekana Keane atasaini mkataba wa miaka mitano na atakuwa akilipwa mshahara wa Pauni 80,000 kwa wiki.
Vilevile inadaiwa tayari ashapimwa afya yake na kinachongojwa tu kwa sasa ni pande zote husika kutia saini mkataba na kuutangaza rasmi.

Na wakati huohuo, Msenegali machachari wa Klabu ya Bolton, El Hadji Diouf, leo yupo Sunderland akikaguliwa afya yake kabla hajasaini mkataba wa uhamisho wa Pauni milioni 2 na nusu.
Diouf, miaka 27, aliingia Bolton mwaka 2005 akitokea Liverpool.
Tayari Meneja wa Sunderland Roy Keane ameshawasaini wachezaji wawili kutoka Tottenham ambao ni Teemu Tainio na Pascal Chimbonda.
Roy Keane anadaiwa vilevile yuko mbioni kuwasaini wachezaji wengine wawili kutoka Tottenham na wanaotajwa ni Steed Malbranque na Younes Kabul.

No comments:

Powered By Blogger