Saturday 2 August 2008


THURAM ASTAAFU SOKA KWA UGONJWA WA MOYO!!!!!!
Lilian Thuram, beki wa zamani wa Ufaransa, ametangaza kustaafu soka kwa sababu ya kuwa na ugonjwa wa moyo.
Thuram, mwenye umri wa miaka 36, alitegemewa kujiunga Klabu ya Ufaransa Paris St-Germain mwezi Juni mwaka huu lakini akagunduliwa ana maradhi ya moyo kwenye ukaguzi wa kawaida wa afya wa kabla ya kusaini mkataba.
Thuram, ambae alikuwemo kwenye kikosi cha Ufaransa kilichonyakua Kombe la Dunia mwaka 1998, alitangaza kustaafu kuichezea Timu ya Taifa ya Ufaransa mara tu Ufaransa ilipotolewa kwenye mashindano ya EURO 2008
Juni mwaka huu.

No comments:

Powered By Blogger