Friday 1 August 2008

ARSENAL NA LIVERPOOL KUJUA WAPINZANI WAO WA LIGI YA MABINGWA ULAYA LEO!!!!
LEO IJUMAA TAREHE 1 AGOSTI 2008 saa 7 mchana zitapigwa kura kuamua timu zipi zitakutana kwenye Raundi ya Tatu ya Mtoano wa LIGI YA KLABU BINGWA ULAYA.
Timu zilizoingia Raundi hii zimegawanywa makundi mawili ambamo Timu za KUNDI LA KWANZA zitacheza na Timu za KUNDI LA PILI.

KUNDI LA KWANZA: Liverpool; Barcelona; Arsenal; Schalke; Juventus; Mshindi kati ya Rangers au Kaunas; Marseille; Steaua Bucharest; Mshindi kati ya Panathinaikos au Dinamo Tbilisi; Mshindi kati ya IFK Gothenburg au Basle; Olympiacos; Mshindi kati ya Fenerbahce au MTK Hungaria; Shakhtar Donetsk; Mshindi kati ya Anderlecht au BATE; Fiorentina; Spartak Moscow.
KUNDI LA PILI: Atletico Madrid; Mshindi kati ya Sheriff Tiraspol au Sparta Prague; Mshindi kati ya Drogheda au Dynamo Kiev; Levski Sofia; Slavia Prague; Galatasaray; Mshindi kati ya Inter Baku au Partizan Belgrade; Victoria Guimaraes; Mshindi kati ya Domzale au Dinamo Zagreb; Mshindi kati ya Beitar Jerusalem au Wisla Krakow; Standard Liege; Twente Enschede; Mshindi kati ya Tampere au Artmedia Bratislava; Mshindi kati ya Aalborg au Modrica; Mshindi kati ya Brann au Ventspils; Anorthosis Mshindi kati ya Famagusta au Rapid Vienna

Hii ina maana vigogo kama Liverpool, Barcelona, Arsenal, Juventus na kadhalika hawawezi kukutana kwa kuwa wote wako KUNDI LA KWANZA.
Katika raundi hii mechi zitachezwa tarehe 12 na 13 Agosti na marudiano ni tarehe 26 na 27 Agosti kwa mtindo wa nyumbani na ugenini.
Washindi 16 wa mechi hizi watajumuika na timu nyingine 16 ambazo ni Mabingwa wa Nchi na washindi wa pili wa ligi za nchi [Timu kutoka Uingereza ni Mabingwa Man U na washindi wa pili Chelsea] kufanya jumla ya timu 32 zitakazogawanywa makundi manane ya timu 4 kila moja zitakazocheza mtindo wa ligi.
Mechi hizi za makundi zitaanza tarehe 16 Septemba na kumalizika Desemba 10.

No comments:

Powered By Blogger