Saturday 2 August 2008


ADEBAYOR KUBAKI ARSENAL,
GALLAS KUBAKI NAHODHA
Imethibitishwa kwamba mshambuliaji Emmanuel Adebayor amepewa mkataba mwingine ambao una nyongeza ya mshahara kufikia Pauni 70,000 kwa wiki na hivyo kuzima zile tetesi anataka kufuata nyayo za wenzake waliohama Arsenal akina Alexander Hleb, Mathieu Flamini na Gilberto Silva.
Wakati huohuo Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, amethibitisha William Gallas ataendelea kuwa Nahodha wa Arsenal kwa msimu ujao.


Baada ya Arsenal kuporomoka vibaya kiuchezaji wakati LIGI KUU UINGEREZA inaelekea ukingoni habari zilizagaa kwamba Gallas atatemwa unahodha kwenye msimu huu unaokuja.


BLACKBURN WAMSAINI MCHEZAJI BORA WA MWAKA WA CHILE
Meneja wa Blackburn, Paul Ince, ametamka kwamba klabu yake imempata Mchezaji Bora wa Chile kiungo Carlos Villanueva [miaka 22] kwa mkopo wa mwaka mmoja kutoka kwa Klabu ya Audax Italiano ya Chile.
Mchezaji huyu anategemewa ataziba pengo lililoachwa na David Bentley aliehamia Tottenham hivi juzi.

No comments:

Powered By Blogger