Tuesday 29 July 2008

UHAMISHO.....ni rasmi sasa!!!!!!!

ROBBIE KEANE YUKO LIVERPOOL!!

Robbie Keane wa Tottenham amehamia Liverpool kwa dau la Pauni milioni 20. Keane amesaini mkataba wa miaka mitano na atakuwa akilipwa mshahara wa Pauni 80,000 kwa wiki.
Liverpool ni Klabu ya sita kwa Keane baada ya kuzichezea Klabu za Wolves, Coventry, Inter Milan na Leeds kabla ya kuhamia Tottenham mwaka 2002.

...............................DIOUF YUKO SUNDERLAND!!!

Nae Msenegali machachari, El Hadji Diouf, rasmi ametua Sunderland kwa uhamisho wa Pauni milioni 2 na nusu kutoka Bolton. Diouf, miaka 27, aliingia Bolton mwaka 2005 akitokea Liverpool.
Tayari Meneja wa Sunderland Roy Keane ameshawasaini wachezaji wawili kutoka Tottenham ambao ni Teemu Tainio na Pascal Chimbonda.

......................PENGO LA DIOUF BOLTON LAZIBWA!!!!!!!!!!!!!!

Baada ya kumpoteza Diouf, Bolton tayari wamepata mtu wa kuziba pengo baada ya kumsajili Winga Mdachi ambae ni mzaliwa wa Ghana Mustapha Riga kwa mkataba wa miaka mitatu.
Mustapha Riga aliichezea Timu ya Taifa ya Uholanzi ya Vijana wa chini ya miaka 21 na ametokea Klabu ya Spain Levante ambayo msimu uliopita imeshuka daraja.

No comments:

Powered By Blogger