Wednesday 30 July 2008


UHAMISHO LIGI KUU UINGEREZA WAPAMBA MOTO!!!!!!!!!!!
Malbranque apimwa afya Sunderland................Atakuwa mchezaji wa tatu toka Tottenham kutua Sunderland!
Steed Malbranque, kiungo mwenye umri wa miaka 28, leo amepimwa afya yake Klabuni Sunderland na endapo mambo yataenda sawa basi atakuwa mchezaji wa tatu kutoka Tottenham kuchukuliwa na Sunderland ndani ya wiki moja.
Wengine waliokwenda Sunderland kutoka Tottenham wiki hii ni beki Pascal Chimbonda na kiungo Teemu Tainio.
Ilitegemewa vilevile beki mwingine wa Tottenham Younes Kaboul angekwenda Sunderland lakini sasa inaelekea atajiunga na Portsmouth.

Stoor atua Fulham!
Fulham imemnunua mchezaji wa Kimataifa wa Sweden Fredrik Stoor kwa mkataba wa miaka mine kutoka Klabu ya Norway ya Rosenberg.
Stoor ni beki wa pembeni na alicheza mechi zote za Sweden kwenye EURO 2008.



Ben Haim aenda Man City!
Beki Myahudi Tel Ben Heim amehamia Manchester City kutoka Chelsea kwa dau ambalo halikutangazwa. Ben Heim alijiunga Chelsea msimu uliopita lakini uchezaji wake ulikuwa wa nadra kwani alishindwa kupata namba ya kudumu kwani Chelsea siku zote walikuwa wakiwapanga John Terry na Ricardo Carvalho.

No comments:

Powered By Blogger