Monday 11 August 2008


WAFAHAMU WACHEZAJI WAPYA WA MAN U: NI NDUGU MAPACHA WAWILI KUTOKA BRAZIL!!!!
NI FABIO DA SILVA NA RAFAEL DA SILVA!!!
Fabio na Rafael Da Silva ni ndugu ambao ni mapacha waliozaliwa tarehe 9 Julai 1990 huko Petropolis, Rio de Janeiro, Brazil.
Ni vijana wenye vipaji sana na ni wachezaji wapya wa Manchester United.
Mapacha hawa hucheza kama mabeki wa pembeni mmoja kulia na mwingine kushoto na Manchester United waliwaibua kutoka Klabu ya Fluminense ya Brazil baada ya kuwaona wakicheza na kung’ara kwenye Timu ya Vijana ya Fluminense kwenye mashindano ya vijana huko Hong Kong mwaka 2005.
Mapacha hawa wameshachezea Timu ya Taifa ya Brazil ya Vijana chini ya miaka 17 na walijiunga na Manchester United Januari mwaka huu. Walishindwa kuanza kuichezea Man U mara baada ya kujiunga kwani maombi yao ya kibali cha kazi yalikwama kwa sababu yalitakiwa yawasilishwe kabla ya Januari.
Lakini walipotimiza miaka 18 [Julai 9, 2008] walikuwa huru kupata kibali cha kimataifa na wakaanza rasmi kuichezea Man U wiki iliyopita kwenye mechi ya kirafiki dhidi ya timu ya Peterborough ambayo Meneja wake ni mtoto wa Meneja wa Man U Sir Alex Ferguson.

Katika mechi hiyo Man U walishinda 2-0 na mashabiki wote walikiri mapacha hao ni hazina.
Jana, hapo uwanjani Wembley, kugombea NGAO YA HISANI ambayo Man U waliwashinda Portsmouth, Fabio na Rafael Da Silva walikuwa miongoni mwa wachezaji wa akib
a wa Man U.

No comments:

Powered By Blogger