Saturday 28 February 2009

CARLING CUP: Jumapili Fainali- Manchester United v Tottenham
Mabingwa Watetezi Kombe la Carling, Tottenham, Jumapili saa 12 jioni [bongo taimu] watajitupa Uwanjani Wembley, mjini London, kupambana na Mabingwa wa England, Ulaya na Dunia, Manchester United, kuwania Kombe la Carling.
Meneja wa Man U, Sir Alex Ferguson, kawaida huchanganya kikosi chake kwenye Kikombe hiki Chipukizi na Maveterani na tayari ameshaambia Vijana Danny Welbeck na Darron Gibson kuwa wataanza Fainali hiyo ila amepata pigo baada ya kugundulika Chipukizi Rafael Da Silva hawezi kucheza kwa kuwa ana ufa mdogo kwenye mfupa wa enka na atakuwa nje ya uwanja kwa mwezi mmoja.
Wachezaji wa Tottenham Robbie Keane, Wilson Palacios, Carlo Cudicini na Pascal Chimbonda wote hawaruhusiwi kucheza kwani walishacheza Kombe hili na Timu zao za zamani kabla ya kuhamia Tottenham msimu huu.
Vilevile, Mshambuliaji Chipukizi Frazier Campbell, haruhusiwi kucheza kwani bado ni Mchezaji wa Man U na yupo Tottenham kwa mkopo tu.
Akizungumzia mechi hii, Ferguson alisema: 'Bila shaka tunataka kushinda Fainali hii lakini ukweli ni kwamba umuhimu kwetu ni LIGI KUU na UEFA CHAMPIONS LEAGUE. Jumatano tunacheza LIGI KUU ugenini na Newcasle na hiyo ni mechi muhimu sana kuliko hii Fainali! Hivyo ntachaguwa Kikosi Jumapili huku nikifikiria Jumatano pia!'
Nae Meneja wa Tottenham, Harry Redknapp amesema: 'Tunacheza na Timu Bora! Juzi walipocheza na Inter Milan walitisha! Lakini tuna Wachezaji wazoefu na bahati ikituangukia, tutacheza vizuri!'

MECHI ZA LIGI KUU England WIKIENDI:
Jumamosi, Februari 28
[saa 9.30 mchana bongo taimu]
Everton v West Bromwich
[saa 12]
Arsenal v Fulham
Chelsea v Wigan
Middlesbrough v Liverpool
Jumapili, Machi 1
[saa 9.30]
Hull v Blackburn
West Ham v Man City
[saa 10.00]
Bolton v Newcastle
[saa 12]
Aston Villa v Stoke City

No comments:

Powered By Blogger