Sunday 22 February 2009

UEFA CHAMPIONS LEAGUE: Yarudi tena kilingeni, Jumanne na Jumatano Viwanja Ulaya kuwaka moto!!!

Mashindano ya kugombea Klabu Bingwa Ulaya yanarudi tena uwanjani kuanzia Jumanne ikiwa sasa ni hatua ya Mtoano kati ya Timu 16 zilizobaki ambazo zitacheza nyumbani na ugenini.
Mabingwa Watetezi Manchester United watakuwa wageni wa Inter Milan huko Italia, Timu inayoongozwa na aliekuwa Meneja wa Chelsea Jose Mourinho.
Timu nyingine za LIGI KUU England zilizokuwemo kwenye hatua hii ya mtoano ni Chelsea, Liverpool na Arsenal.
Arsenal watakuwa kwao Emirates kuwakaribisha AS Roma ya Italia, Chelsea yuko nyumbani Stamford Bridge kumkaribisha Juventus ya Italia na Liverpool watakuwa huko Spain Uwanja wa Bernabeau nyumbani kwa Real Madrid.
RATIBA KAMILI:
Jumanne, Februari 24
Arsenal v AS Roma

Atletico Madrid v FC Porto

Inter Milan v Man U

Lyon v Barcelona

Jumatano, Februari 25
Chelsea v Juventus

Real Madrid v Liverpool

Sporting v Bayern Munich

Villareal v Panathinaikos

No comments:

Powered By Blogger