Sunday 22 February 2009

Man U 2 Blackburn 1: Man U wako pointi 8 mbele, Liverpool wacheza leo!!!

Jana Manchester United wakiwa nyumbani Old Trafford waliifunga Blackburn, timu ambayo siku zote huwawekea ngumu, mabao 2-1 kwa mabao ya Wayne Rooney na Cristiano Ronaldo.
Bao la Blackburn, ambalo ni la kwanza Man U wanafungwa kwenye LIGI KUU tangu Sami Nasri wa Arsenal atoboe nyavu zao Novemba 8 mwaka jana, lilifungwa na Mshambuliaji wao hatari Roque Santa Cruz.
Refa Howard Webb aliiacha mechi hii ikiwa na malumbano baada ya kulikataa bao la wazi la Man U lililofungwa na Johnny Evans kwa kichwa kufuatia kona na 'kuwanyima' penalti Blackburn pale ilipodaiwa Pedersen alivutwa na Rafael.
Hata hivyo Man U wangeweza kutoka na ushindi mnono endapo nafasi za wazi zilizotua kwa Ronaldo, Rooney na Berbatov zingetumiwa vilivyo.
Leo Liverpool wanajimwaga uwanjani kwao Anfield kupambana na mahasimu wakubwa wa Man U, Manchester City, wakipigania kupunguza pengo lilopo la pointi 8 kati yao na Man U.
Liverpool wataingia uwanjani bila ya tegemezi Steven Gerrard ambae ni majeruhi na Xabi Alonso aliefungiwa mechi hii.
MECHI NYINGINE ZA LEO NI:
Fulham v West Ham
Newcastle v Everton

No comments:

Powered By Blogger