Monday 23 February 2009

INTER MILAN v MAN U: Ronaldo: 'Ni kuua au kuuawa!!!'
-Nae Beckham ashabikia Man U: 'Watashinda! Ntaenda uwanjani kuongea na timu!'


Mchezaji Bora Duniani, Cristiano Ronaldo, anaamini timu yake Manchester United ni bora na ina uzoefu mkubwa kupita wapinzani wao wa kesho kwenye pambano la mtoano la UEFA CHAMPIONS LEAGUE, Inter Milan ya Italia, litakalochezwa huko Milan, Italia.
'Litakuwa pambano gumu kwani wao wanaongoza ligi ya kwao SERIE A lakini sisi ni bora na tuna uzoefu mkubwa,' Ronaldo alisema. 'Sisi ni Mabingwa watetezi na tuna Wachezaji wazuri sana! Sasa tupo hatua ya kuua au kuuawa!'
Nae Mchezaji wa zamani wa Man U ambae kwa sasa yuko AC Milan ya Italia ambao ni wapinzani wa jadi wa Inter Milan, David Beckham, ambae alicheza mechi kati ya wapinzani hao wiki mbili zilizopita mechi ambayo Inter iliifunga AC Milan 2-1, amesema: 'Inter wana Wachezaji wazuri wenye nguvu na kasi na hasa Fowadi yao ni hatari na inamudu vyema kumiliki mpira. Ukiidhibiti Fowadi hiyo basi una nafasi! Man U kwa sasa wana timu nzuri, Defensi yao ni ngome kubwa na Fowadi yao hatari sana!'
Beckham aliongeza: 'Kama mpenzi wa Man U, nipo upande wao na kama Mchezaji wa AC Milan, nipo upande wa Man U! Nitaenda kwenye mechi na nitaongea na Wachezaji wa Man U na Sir Alex Ferguson.'
Beckham alimalizia: 'Man U wanastahili kushinda lakini pengine ninawapendelea kwani mie ni shabiki mkubwa na naipenda!'
Inter Milan kwa sasa inaongozwa na Meneja Jose Mourinho ambae alikuwa Chelsea na kuwepo kwake kunaleta kumbukumbu ya mapambano akiwa Chelsea na misuguano yake na Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson. Akiwa Chelsea aliiwezesha timu hiyo kuwa Mabingwa wa LIGI KUU mara mbili mfululizo.
Inter Milan ina Wachezaji mahiri na maarufu kama kina Toldo, Cordoba, Zanetti, Maicon, Marco Materazzi, Chivu, Luis Figo, Patrick Viera, Cambiasso, Sulley Muntari, Alesandro Mancini, Zlatan Ibrahimovic, Adriano.
Kikosi cha Man U kilichosafiri leo kwenda Italia ni: Van der Sar, Kuszczak, Ferdinand, Evra, O'Shea, Evans, Fabio, Eckersley, Giggs, Park, Carrick, Nani, Scholes, Possebon, Gibson, Fletcher, Ronaldo, Rooney, Bebatov, Tevez, Welbeck

LIGI KUU England: Baada ya Man City kuwavuta jezi, Benitez bado aota Ubingwa lakini Mark Hughes wa Man City awapa ukweli!!

Meneja wa Liverpool, Rafael Benitez, baada ya jana timu yake kutoka droo 1-1 na Man City na hivyo kubaki nyuma ya Manchester United kwa pointi 7 huku zimebaki mechi 12, bado hajakata tamaa na anaamini wanaweza kutwaa ubingwa wakishinda mechi zao zote zilizobaki ikiwemo ile watakayokwenda Old Trafford nyumbani kwa Man U kupambana na Mabingwa hao tarehe 14 Machi 2009.
'Si rahisi' Benitez alikiri na kuongeza. 'Kitu muhimu tushinde mechi zetu pamoja na ile ya Old Trafford!'
Lakini Meneja wa Man City Mark Hughes ambae aliwahi kuwa Straika hatari wa Man U, mbali ya timu yake jana kuipunguza kasi Liverpool kwa droo ya 1-1, pia amewakatisha tamaa kwa kutamka: 'Si kitu rahisi Liverpool kuwa Bingwa! Inabidi Man U ateleze na hicho si kitu rahisi! Inabidi wapoteze mechi 3 na Liverpool ashinde zote!'

No comments:

Powered By Blogger