Friday 27 February 2009

Villa, Tottenham nje, Man City wasonga!!!

Aston Villa, wakipumzisha nusu ya kikosi chao thabiti, walipigwa goli 2-0 na CSKA Moscow mjini Moscow na hivyo kutolewa nje ya UEFA CUP kwa jumla ya mabao 3-1. Mechi ya kwanza ilikuwa 1-1.
Nao Tottenham walitoka suluhu 1-1 na Shakhtar Donetsk na kuyaaga mashindano kwani walifungwa 2-0 mechi ya kwanza.
Timu pekee ya England iliyofuzu ni Manchester City iliyoshinda 2-1 na kuitoa FC Copenhagen kwa jumla ya mabao 4-3.
Raundi ijayo Manchester City itakutana na Aalborg ya Denmark.

No comments:

Powered By Blogger