Sunday 22 February 2009

Liverpool chupuchupu, waambulia sare!!! Sasa wako nyuma ya Man U kwa pointi 7!!!!

Liverpool wakiwa ngomeni kwao Anfield walipigana kufa na kupona kujinusuru wasifungwe na Manchester City timu ambayo haijawahi kushinda ugenini tangu Agosti mwaka jana baada ya Craig Bellamy kuifungia Man City bao dakika ya 4 kipindi cha pili.
Liverpool wakijitutumua walisawazisha kupitia Dirk Kuyt dakika ya 78.
Matokeo hayo yanawafanya Liverpool wawe na pointi 55 wakiwa pointi 7 nyuma ya Manchester United wenye pointi 62.

Fulham 2 West Bromwich Albion 0

Mabao ya Bobby Zamora na Andy Jonhson yamewapa ushindi wa 2-0 Fulham dhidi ya timu ya mwisho kwenye LIGU KUU West Bromwich Albion.

No comments:

Powered By Blogger