Thursday 26 February 2009

Man City, Aston Villa na Tottenham leo wanajimwaga UEFA CUP kuwania nafasi ya Timu 16

Leo usiku Timu za LIGI KUU England Manchester City, Aston Villa na Tottenham wanajitupa uwanjani kuwania kuingia Raundi ya Timu 16 kwenye Kombe la UEFA mechi za leo zikiwa marudiano ya mechi za duru la kwanza lililochezwa wiki iliyokwisha.
Manchester City leo wako nyumbani kurudiana na FC Copenhagen na timu hizi zilitoka sare 2-2 katika mechi ya kwanza.
Aston Villa wako ugenini kurudiana na CSKA Moscow na mechi kati yao ya kwanza iliisha droo 1-1.
Tottenham, ingawa leo wako nyumbani, ndio wenye kibarua kikubwa kwani kwenye mechi ya kwanza walikutwa mabao 2-0 na Timu ya Ukraine Shakhtar Donetsk.
Mbali ya mechi hizi zinazohusu Timu za LIGI KUU England pia kuna mechi nyingine za UEFA CUP zinazohusisha timu 26 kwani raundi hii ina jumla ya timu 32.
Baadhi ya mechi za kuvutia za leo ni zile za marudiano kati ya Ajax na Fiorentina, AC Milan v Werder Bremen, Depotivo La Coruna v Aab, Galatasaray v Bordeaux, Valencia v Dynamo Kiev.

No comments:

Powered By Blogger