Saturday 28 February 2009

Refa Peter Walton aiomba Sheffield United msamaha kwa makosa katika uchezeshaji yalioipa Hull City ushindi!!

Refa Peter Walton ambae ni mmoja wa Marefa wanaochezesha LIGI KUU England amempigia simu Bosi wa Sheffield United Kevin Blackwell ili kumuomba msamaha kufuatia makosa makubwa yaliyofanywa kwenye mechi ya Kombe la FA kati ya Hull City na Sheffield United iliyochezwa Alhamisi na Hull City wakaibuka washindi 2-1.
Mshika Kibendera aliashiria kwa Mwamuzi Peter Walton kuwa bao la kwanza mpira ulivuka mstari kufuatia kichwa kibovu cha Mlinzi wa Sheffield United Kyle Naughton kugonga mwamba wa juu wa goli na kudunda mstarini na kutoka nje ya goli.
'Tulipoteza mechi ambayo hatukufungwa! Lile goli la kwanza mpira haukuvuka mstari!' Kevin Blackwell alilalamika. 'Na Refa alitunyima penalti ya wazi! Lakini huyu Refa ni mwungwana kwani amenipigia simu kuomba radhi baada ya kuona marudio ya mechi kwenye video na kuungama walikosea! Hakutakiwa kuomba radhi lakini ameomba, ni utu wa hali ya juu!'

No comments:

Powered By Blogger