Wednesday 23 December 2009

Anelka kuzikosa mechi za Ligi Kuu Xmas!!
Mshambuliaji wa Chelsea Nicolas Anelka atazikosa mechi za Chelsea za Ligi Kuu za Desemba 26 watakapocheza ugenini na Birmingham na ile ya Desemba 28 watakapoivaa Fulham katika dabi ya Timu za Magharibi ya London kwa sababu ni majeruhi.
Anelka hakucheza mechi ya Jumapili iliyopita ya Ligi Kuu Chelsea walipotoka sare na West Ham kwa vile ameumia mguu na sasa tatizo hilohilo limemfanya aendelee kuwa nje.
Sasa Chelsea wamesema wanategemea Anelka kuanza kucheza kwenye mechi ya Kombe la FA hapo Januari 3 watakapocheza na Watford.
Chelsea pia watamkosa Mshambuliaji wao mkubwa Didier Drogba ambae anatakiwa ajiunge na Timu ya Taifa ya Ivory Coast kabla ya mwisho wa Desemba kwa ajili ya matayarisho ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazochezwa huko Angola kuanzia Januari 10.
Ivory Coast inategemewa kupiga Kambi yake ya mazoezi Nchini Tanzania mwanzoni mwa Januari ambako itakutana na Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, katika mechi mbili za kujipima nguvu.
Diouf apata kibali kuchezea Man U!!!
Mchezaji kutoka Senegal, Mame Biram Diouf, miaka 22, amepewa kibali cha kazi na hivyo kuruhusiwa kuichezea Manchester United kuanzia Januari.
Diouf alisajiliwa na Manchester United kabla msimu huu kuanza kutoka Klabu ya Molde ya Norway lakini ikabidi aendelee kuichezea Molde kwa mkopo kwa sababu ya kukosa kibali cha kazi.
Tangu wakati huo, ameshaichezea Molde mechi 12 na kufunga mabao manne na kufanya idadi yake ya magoli kwa Klabu ya Molde kuwa ni 33 katika mechi 75 alizoichezea.
Bosi wa Man U, Sir Alex Ferguson, amemsifia Diouf ambae ameshaichezea Senegal mara moja, kwa kutamka: “Anafanya mazoezi na sisi na anafurahisha na kuvutia! Klabu yetu ni bora kwa kuvumbua vipaji na kuvikuza! Yeye ana miaka 22 tu na anaonekana ni bora!”

No comments:

Powered By Blogger