Saturday 26 December 2009

Kitendawili cha Rio kurudi uwanjani!!!
Rio Ferdinand anasumbuliwa na tatizo la mgongo ambalo husababisha hata kuumwa kwa misuli ya miguu yake na ugonjwa huu umemweka nje ya uwanja tangu mwishoni mwa Oktoba na kusababisha kuzikosa mechi za Klabu yake Manchester United 13 na mpaka sasa Klabu yake haijui lini atarudi uwanjani.
Sir Alex Ferguson, Meneja wa Man U, amesema Rio ataonekana muda si mrefu ingawa hakusema lini ila aligusia tu kuwa wiki mbili zilizopita alipigwa sindano na baada ya wiki moja akaanza mazoezi kweye jim na bado wanamwangalia maendeleo yake.
Siku chache zilizopita, mwenyewe Rio alitamka, wakati wa ufunguzi wa Mfuko wake wa Hisani, kuwa nafasi yake kwenye Kikosi cha England kitakachoenda Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini mwezi Juni haiko mashakani.
Lakini, wakati Ligi Kuu leo inatimiza kufikia hatua ya Nusu yake kwa Timu kucheza mechi 19 kati ya 38 wanazotakiwa kucheza, Wadau wanajiuliza kuhusu Rio na Ferguson akazungumza: “Rio yuko imara. Hajaonyesha athari zozote kisaikolojia kuhusu kuumia kwake. Lakini nina hakika yeye kama Mchezaji ana usongo mkubwa wa kutaka kucheza mechi hasa wakati huu kwenye mvutano mkubwa kuelekea Ubingwa!”

No comments:

Powered By Blogger