Saturday 26 December 2009

Benitez aungama: “Torres hayuko fiti!!!!”
Meneja wa Liverpool Rafa Benitez amekubali kuwa Mshambuliaji wake nyota Fernando Torres hayuko fiti kucheza kila mechi na wanalazimika kumchunguza kwanza na halafu waamue kama acheze au la.
Msimu huu, Torres amekuwa nje mara kwa mara na kuna uvumi kuwa inabidi afanyiwe operesheni ya kutibu ngiri [hernia].
Katika mechi ya mwisho waliyocheza Liverpool na kufungwa 2-0 na Portsmouth kwenye Ligi Kuu, Torres alicheza chini ya kiwango lakini katika mechi ya leo ya Desemba 26 watakapocheza na Wolves kwenye Ligi Kuu, Mchezaji huyo anategemewa kuanza.
Liverpool, ambao wako pointi 8 nyuma ya Timu 4 za juu, wanakabiliwa na mechi ngumu 3 mfululizo baada ya mechi ya leo, kwenye Ligi Kuu, watacheza na Aston Villa, iliyo nafasi ya 4 kwenye Ligi, kisha watacheza na Reading kwenye Kombe la FA na baada ya hapo watapambana kwenye Ligi Kuu na Timu ya 5 kwenye Ligi, Tottenham.
Benitez anahaha kuhakikisha Straika wake yuko fiti lakini amekiri: “Ni lazima tumwangalie na kuhakikisha anacheza akiwa fiti tu!
Wakati huohuo, Benitez amekanusha taarifa kuwa alifanya mazungumzo na Nahodha wake Steven Gerrard ili kujadili kushuka kwa kiwango chake na kutojiamini kwake.
Mwenyekiti Arsenal aishambulia Barca!!!
Mwenyekiti wa Arsenal Peter Hill-Wood ameishambulia vikali Barcelona kwa kuwandama Nahodha wao Cesc Fabrega, miaka 22, na kujaribu kumrubuni ajiunge na Barcelona.
Mara kwa mara Barcelona imekuwa ikihusishwa na kumnunua Fabregas ambae alianza mpira akiwa kwenye Timu ya Vijana ya Barcelona na kisha kujiunga Arsenal.
Ingawa Real Madrid nao wanatajwa kutaka kumnunua Fabregas lakini ni Barcelona wakiongozwa na Rais wao Joan Laporta ndio vinara wa kumrubuni Kiungo huyo wa Arsenal mwenye asili ya Spain.
Na kauli za hivi karibuni za Joan Laporta zimemkera mno Mwenyekiti wa Arsenal, Peter Hill-Wood, aliefoka: “Nimechoka na uhuni huu wa Barcelona na upumbavu wao! Cesc ana Mkataba wa muda mrefu na mzuri na sisi! Yuko na sisi miaka 7 sasa na hana nia ya kuondoka! Hatuwezi kuwazuia kuongea ovyo lakini huu ni upuuzi uliokithiri!!”

No comments:

Powered By Blogger