Friday 13 June 2008

EVRA AONGEZA MKATABA
Mlinzi alieng'ara sana msimu uliopita, Mfaransa Patrice Evra, ameongezewa mkataba na klabu yake ya Manchester United na hivyo atabaki OLD TRAFFORD hadi mwaka 2012.
Evra, ambae kwa sasa yuko kwenye kikosi cha Ufaransa EURO 2008, ameshashinda LIGI KUU UINGEREZA mara 2 na KLABU BINGWA ULAYA mara moja tangu ajiunge MAN U.
Akiwa mwenye furaha, Evra alisema: 'Misimu miwili ilopita ilikuwa kama ndoto nzuri kwangu! Ni furaha na sifa kubwa kuwa mmoja wa timu hii bora na kufundishwa na Sir Alex Ferguson na wasaidizi wake.'

No comments:

Powered By Blogger