Tuesday 10 June 2008





FRANCE 0
ROMANIA 0!

Katika mechi ilyopooza, Ufaransa na Romania zilitoka sare ya 0-0.

Kwenye mechi iliyofuata ya Kundi hilo C, kundi ambalo wengi wamelibatiza 'KUNDI LA KIFO', Uholanzi ilifanya mauaji makubwa baada ya kuibamiza Italia kwa mabao 3-0. Goli lenye utata la Ruud Van Nistelrooy kwenye dakika ya 26 na la pili la Wesley Sneijder dakika ya 31 liliwafanya Uholanzi kuwa mbele 2-0 hadi mapumziko.
Giovanni van Bronckhorst alipachika bao la tatu kwa kichwa dakika ya 80 na kuwaacha Uholanzi wakioongoza Kundi C.

LEO NI MECHI ZA KUNDI D wakati SPAIN na URUSI zitapocheza saa 1 usiku huko Innsbruck na watafuatiwa na UGIRIKI na SWEDEN mjini Salzburg saa 3 dakika 45.

No comments:

Powered By Blogger