Tuesday 10 June 2008

SAKATA LA RONALDO
MAN U wawashitaki REAL FIFA!
Mabingwa wa LIGI KUU UINGEREZA na ULAYA, MAN U wamewashitaka REAL MADRID kwenye bodi inayoongoza soka duniani FIFA kwa kumrubuni mchezaji wao Ronaldo kinyume na taratibu.
Taarifa iliyotolewa na MAN U iliripoti:
'Tarehe 27 MEI 2008, United ilitangaza rasmi nia yake kuishitaki Real endapo wataendelea kujihusisha na hatma ya baadae ya Ronaldo. Kwa bahati mbaya, Real wameendelea kumsakama mchezaji wetu. Klabu inaona haina njia ila kuwasilisha malalamiko yetu kwa FIFA.'
FIFA imethibitisha kupokoa kabrasha la malamiko hayo.

No comments:

Powered By Blogger