Friday 13 June 2008


UVUMI….wachezaji kuhama na…………..!!!



  • Meneja mpya wa Chelsea Scolari ana kitita cha Mamilioni ya Pauni za Kiingereza alizopewa na mmiliki Abramovitch kuwabeba Fernando Torres, Frank Ribery na Kaka.

  • Nyota wa Arsenal Emmanuel Adebayor ana shauku kuhama Emirates Stadium kwenda AC Milan.

  • Nia ya Arsenal kumsaini kiungo wa Marseille Samir Nasri inaelekea itapigwa chini na Atletico Madrid ambao nao wanamtaka mchezaji huyo.

  • Sir Alex Ferguson tayari ameingia vitani na Luiz Felipe Scolari kwa kumtaka Meneja huyo mpya wa Chelsea ambaye kwa sasa anaiongoza Ureno kwenye EURO 2008 aache kumshawishi Cristiano Ronaldo kuhamia Real Madrid.

  • Na baada ya kuondoka Scolari kwenda Chelsea, Ureno itamchukua Meneja msaidizi wa Man U Carlos Queiroz ili awe Meneja wa Ureno.

MATOKEO KUNDI B:


Croatia 2-1 Germany


Croatio wametua Robo Fainali ya EURO 2008 baada ya mabao ya Darijo Srna na Ivica Olic kuwaua Ujerumani. Lukas Podolski alifunga bao moja kwa Ujerumani.


Austria 1-1 Poland
Refa wa Kiingereza Howard Webb jana aliwaokoa wenyeji wenza AUSTRIA kutolewa EURO 2008 kama wenzao USWISI baada ya kuwapa penalti dakika za majeruhi ambayo Ivica Vastic alifunga na kuwawezesha kutoka sare 1-1 na Poland na hivyo kubaki wanasuasua EURO 2008.
Nalo goli la kipindi cha kwanza la Poland lililofungwa na Roger Guerreiro, Mpoland aliezaliwa Brazil, lilikuwa la utata kwani mfungaji alionekana dhahiri ameotea.


LEO KUNDI C ['kundi la kifo']:


Saa 1 usiku: ITALIA vs RUMANIA
Saa 3.45 usiku: UHOLANZI vs UFARANSA



No comments:

Powered By Blogger