Sunday 8 June 2008


Ronaldo hajaamua 'hatma yake'
Jana baada ya kuiongoza nchi yake URENO kuishinda UTURUKI 2-0 kwenye mechi yao ya ufunguzi ya EURO 2008, Cristiano Ronaldo amesema hajaamua nini hatma yake na atatoa kauli baada ya Ureno kumaliza EURO 2008.
Real Madrid wanamuwinda staa huyo kwa udi na uvumba huku Manchester United waking’ang’ania hawataki katakata kusikia biashara hiyo wakidai Ronaldo bado ana mkataba wa miaka minne na wametishia kuishtaki Real FIFA kwa kumrubuni mchezaji huyo.
Hata hivyo, mchezaji mwenzake Ronaldo katika Timu ya Taifa ya Ureno Ricardo Carvalho, ambae ni beki wa Chelsea, anaamini Ronaldo atabaki Man United.
Hiyo jana, Carvalho aliongea:'Ana furaha Man U na atabaki huko'

No comments:

Powered By Blogger