Sunday 26 October 2008

Chelsea 0 Liverpool 1

Ile rekodi ya Chelsea ya kutokufungwa mechi 86 za LIGI KUU kwenye ngome yao, uwanja wa nyumbani Stamford Bridge, leo imekwenda na maji baada ya kufungwa na Liverpool bao 1-0.
Mara ya mwisho kwa Chelsea kufungwa hapo kwao ilikuwa ni Februari, 2004 walipofungwa na Arsenal.
Sasa Liverpool wanaongoza ligi wakiwa na pointi 23.
Bao la ushindi la Liverpool lilifungwa na Xabi Alonso kwenye dakika ya 10 baada ya shuti lake kumbabatiza Beki wa Chelsea Bosingwa na kumpoteza maboya Kipa Petr Cech.

No comments:

Powered By Blogger