Friday 31 October 2008

Gallas majeruhi!

Nahodha wa Arsenal William Gallas ataikosa mechi ijayo na Stoke City siku ya Jumamosi baada ya kuumia kufuatia habari alizozitoa Meneja wake Arsene Wenger ambae pia amethibitisha nae Eboue ni majeruhi.

Carvalho nje!

Beki wa kutumainiwa wa Chelsea Ricardo Carvalho atakuwa nje ya uwanja kwa wiki tatu baada ya kuumia goti katika mechi timu yake iliyoishinda Hull City juzi kwa mabao 3-0.

Tevez ni muhimu kwetu-Sir Alex Ferguson!

Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, ametamka Carlos Tevez ni bado mchezaji muhimu sana kwa timu yake ingawa hajaanza mechi nyingi hivi karibuni.
Katika mechi ya juzi ambayo Man U waliifunga West Ham 2-0, Tevez alianza na Rooney alikuwa benchi.
Sir Alex Ferguson amesisitiza ni bado muhimu sana na kwamba kwa sasa tatizo ana mastraika watatu na ni wawili tu ndio wanaoweza kucheza kwa wakati mmoja, bila shaka, akimaanisha mastraika hao ni Berbatov, Rooney na Tevez.

Adebayor akiri: 'Hatuwezi kuwa mabingwa!'

Baaada ya kuona timu yake Arsenal ikiporwa pointi sekunde ya mwisho ya mechi na Tottenham wakati zilipotoka sare ya bao 4-4 baada ya Aaron Lennon wa Tottenham kuisawazishia, Adebayor amelalamika: 'Huwezi kuwa bingwa namna hii!! Huu ni ukweli!'

No comments:

Powered By Blogger