Saturday 1 November 2008

Wenger adharau ripoti ngumi zilifumuka kati ya Wachezaji wake baada ya sare na Tottenham!

Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, amekanusha ripoti zilizozagaa kwamba Wachezaji wake waligombana katika chumba cha kubadilishia nguo uwanjani kwao Emirates Stadium mara baada ya mechi na Tottenham ambayo iliisha suluhu 4-4 baada ya Tottenham waliokuwa nyuma kwa bao 4-2 kusawazisha dakika za mwisho.
Taarifa zilizigaa kuwa Wachezaji waligombana na sasa nyufa zimeanza kujitokeza kwenye timu kitu ambacho Arsene Wenger anabisha.
Baada ya mechi, staa wao Adebayor alikaririwa akidai Arsenal hawawezi kuchukua ubingwa.
Wenger amekanusha kama kuna mifarakano kwa kusema: 'Sote tulisononeka kwa droo ile. Kwenye chumba cha kubadilishia nguo, kila mmoja alivunjika moyo na alikuwa haamini nini kilitokea. Lakini, sisi ni wamoja na tutaibuka na ushindi!'
Arsenal haijatwaa Kombe lolote tangu iliposhinda FA CUP mwaka 2005.

No comments:

Powered By Blogger