Friday 31 October 2008

NI RASMI: BECKHAM ATUA AC MILAN KWA MKOPO!!!

AC Milan ya Italy imethibitisha kuwa David Beckham atajiunga na klabu hiyo kwa mkopo kuanzia Januari 7, 2009.
Beckham, mwenye miaka 33, ni mchezaji wa Klabu ya Marekani ya LA Galaxy ya huko Marekani ambako kwa sasa msimu wa ligi umeisha na utaanza upya mwakani mwezi Aprili.
Ili kujiweka fiti, Beckham ameamua kujiunga na Klabu hiyo ya Italia aweke uhai matumaini yake ya kuendelea kuichezea Timu ya Taifa ya Uingereza ambayo mpaka sasa ameshaiwakilisha mara 108.
Meneja wa England, Fabio Capello, ambae aliwahi kuwa na AC Milan kwa vipindi viwili vya kati mwaka 1991-1996 na 1997-1998 ameunga mkono hatua hiyo ya Beckham kwa kusema: 'Milan wamepata mchezaji bora'
Vilevile Capello aliongeza: 'Nilipokuwa nae Real Madrid alisaini mkataba na LA Galaxy na nikamuacha kwenye kikosi changu lakini kila siku alikuja kufanya mazoezi kwa bidii tu, nikamrudisha! Ni mtu makini sana, mwenye bidii na ingawa watu wanafikiri ni pleiboi nje ya uwanja lakini hilo si kweli hata chembe!'

No comments:

Powered By Blogger