Sunday 26 October 2008

Tottenham wamtimua Ramos na kumchukua Redknapp!

Tottenham Hotspur wamemfukuza kazi Meneja wao Juande Ramos pamoja na Mkurugenzi wa Michezo Damien Comolli na wamemteua Meneja wa Portsmouth Harry Redknapp kuwa Meneja mpya.
Tottenham vilevile imewaachisha kazi Makocha Gus Poyet na Marcos Avarez.
Mechi ya leo ambayo Spurs inacheza na Bolton Makocha Wasaidizi Clive Allen na Alex Inglethorpe ndio watakaosimamia timu.
Mpaka sasa Tottenham ndiio wanashika mkia kwenye LIGI KUU wakiwa na pointi 2 tu katika mechi 8 walizocheza.
Juande Ramos alijiunga na Tottenham Oktoba 2007 akitokea klabu ya Sevilla ya Spain baada ya kufukuzwa kwa Meneja Mholanzi Martin Jol.

MAN U WAKANUSHA KUWA MAZUNGUMZO NA MOURINHO

Manchester United wameziponda taarifa kwamba wapo kwenye mazungumzo na Jose Mourinho ili awe Meneja wao baada ya kustaafu kwa Meneja wa sasa Sir Alex Ferguson.
Jose Mourinho mwenyewe ametamka wiki hii kwamba angependa kurudi tena kwenye LIGI KUU UINGEREZA mkataba wake na Inter Milan ukimalizika mwaka 2011 ingawa hakutaja klabu angeyopenda kwenda.
Nae Sir Alex Ferguson alishatamka kuwa hategemei kuendelea kuwa Meneja wa Man U baada ya mwaka 2010 wakati huo atakuwa ametimiza miaka 24 ya kuwa Meneja wa Man U.
Msemaji wa Manchester United ametamka: ‘Kama tulivyosema mara nyingi, hakuna mazungumzo yeyote ya nani atamrithi Sir Alex Ferguson akistaafu
.’

WALIO KILELENI KUKUMBANA LEO!

Timu za Chelsea na Liverpool zinazoongoza LIGI KUU zikiwa zote zina pointi 20 INGAWA Chelsea yuko mbele kwa idadi makubwa ya magoli zinapambana Stamford Bridge kwenye ngome ya Chelsea.
Stamford Bridge hakika ni ngome kwa Chelsea kwani mpaka sasa hawajafungwa hapo katika mechi 86 za LIGI KUU. Nao Liverpool, mbali ya kuhofia rekodi hiyo ya Chelsea, wao wenyewe wana rekodii mbaya ya kucheza hapo katika mechi za LIGI KUU kwani katika mechi 16 za ligi walizocheza hapo ni mechi moja tu walishinda.
Msimu huu Liverpool wamesha jizolea sifa ya kuwa mafundi wa kushinda mechi wanazotangulia kufungwa kama vile walivyofanya katika mechi zao na Middlesbrough, Manchester United, Manchester City na Wigan.
Nahodha wa Chelsea John Terry aemesema wao wana usongo wa kukata maini Liverpool ili kudhihirisha wao ndio wanaostahili kuwa Mabingwa.
Timu zinaweza kuchaguliwa kutoka kwa Wachezaji wafuatao:
Chelsea:
Cech, Bosingwa, Carvalho, Terry, Bridge, Mikel, Lampard, Deco, Malouda, Anelka, Kalou.
Liverpool: Reina, Arbeloa, Carragher, Agger, Dossena, Riera, Alonso, Mascherano, Gerrard, Kuyt, Keane.

MECHI NYINGINE ZA LEO JUMAPILI 26 OKTOBA 2008:

[saa 12 jioni]

Man City v Stoke City

Tottenham v Bolton

Wigan v Aston Villa

[saa 1 usiku]

West Ham v Arsenal

[saa 2 usiku]

Portsmouth v Fulham

Alex Ferguson adai alimtoa Rooney ili asipewe kadi nyekundu!

Sir Alex Ferguson amedai ilibidi ambadilishe Wayne Rooney katika mechi waliyotoka suluhu na Everton ili kumuokoa asipewe kadi nyekundu na Refa Alan Wiley ambae muda mfupi kabla ya hapo alimpa kadi ya njano Rooney kwa rafu dhidi ya Mikel Arteta, kadi ambayo Ferguson vilevile alidai haikustahili na Refa aliitoa kwa sababu ya shindikizo la watazamaji.
Wayne Rooney ambae alikuwa Mchezaji wa Everton kabla ya kujiunga na Man U kuna wakati alionekana akishika jezi yake na kuibusu huku akiwapungia mashabiki waliokuwa wakimzomea.

No comments:

Powered By Blogger