Monday 27 October 2008

WAFUNGAJI BORA:

Baada ya kila Timu LIGI KUU kucheza mechi 9, kasoro Mabingwa Man U na Fulham wenye mechi ya kiporo kati yao, huku ligi ikongozwa na Liverpool wakifuatiwa na Chelsea kisha Hull City, Arsenal, Aston Villa na Man U, Mfungaji Bora mpaka sasa ni Mshambuliaji toka Afrika Amr Zaki kutoka Misri [pichani] anaechezea Klabu ya Wigan mwenye magoli 7.
Anaefuta ni Mbrazil Robinho wa Man City mwenye goli 6 huku Agbonlahor na Carew wa Aston Villa pamoja na Defoe wa Portsmouth na Torres wa Liverpool wakifuatia wakiwa na magoli matano kila mmoja.
Adebayor [Arsenal], Anelka [Chelsea], Bent [Tottenham], Crouch [Portsmouth], Davies [Bolton], Geovanni [Hull] na Van Persie [Arsenal] wana goli 4 kila mmoja.
Mfungaji Bora wa msimu uliopita Cristiano Ronaldo wa Manchester United, alieanza kucheza hivi karibuni baada ya operesheni ya enka, ana goli 2.

No comments:

Powered By Blogger