Monday 27 October 2008

Sir Alex Ferguson: 'Ronaldo atazidi kuwa bora!'

Baada ya Crsitiano Ronaldo kushinda TUZO YA FifPro WORLD FOOTBALLER OF THE YEAR 2008, Sir Alex Ferguson ametamba Ronaldo atazidi kuwa bora zaidi kwa kuwa bado ana umri mdogo.
Msimu huu, Sir Alex Ferguson ametabiri Ronaldo atafunga magoli 25 kwa kuwa ameanza msimu akitokea kwenye operesheni ya enka. Msimu uliokwisha, Ronaldo alifunga mabao 42.
Ronaldo, mwenye umri wa miaka 23, nae amekiri: 'Bosi wangu Sir Alex Ferguson ni mtu muhimu kwangu. Nipo klabu hii kwa sababu yake! Alinichukua wakati nina miaka 18 tu na amenisaidia sana! Anaheshimu wachezaji wote, anajua kuongea na wachezaji na hiyo ni muhimu. Asilimia 99 ya wachezaji wana uhusiano mzuri na yeye! Ni mtu bora sana! Ni sifa kubwa sana kuwa Manchester United pamoja na yeye, yeye ameshinda kila kitu kwa klabu hii!'
Sir Alex Ferguson alimsifia vilevile Rio Ferdinand ambae pamoja na Ronaldo wapo kwenye TIMU BORA YA 2008 YA FifPro kwa kusema: 'Rio si mlinzi bora tu bali ana uwezo mkubwa wa kugeuza ulinzi kuwa mashambulizi! Hilo alikuwa nalo lakini kwa sasa ni ule uwezo wa kuwa kiongozi na kuwa mstari wa mbele kuhamasisha timu kwa kila kitu!'

No comments:

Powered By Blogger